Je ugonjwa huu unaweza kuambukizwa kutoka kwa binadamu kwenda kwa binadamu?
Hapana. Ugonjwa huu hauenezwi kutoka
binadamu mmoja kwenda kwa mwingine bali ugonjwa huu huenezwa na mbu
aliyeambukizwa na virusi vya homa ya dengue anapomuuma binadamu..
Je,ugonjwa huu unatibika?
Ndio,Ugonjwa wa homa ya dengue
unaweza kutibika kama mgonjwa atapelekwa hospitali mapema na kupatiwa
matibabu ya haraka.Hakuna tiba maalumu ya ugonjwa huu bali mgonjwa
anatibiwa kutokana na dalili zitakazoambatana na ugonjwa huu kama vile
homa, kupungukiwa maji au damu vile vile hadi sasa hakuna chanjo kwa
ajili ya kinga kwa binadamu.
Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya dengue
• Kuangamiza mazalio ya mbu
• Fukia madimbwi ya maji yaliyotuama au nyunyuzia dawa ya kuua vimelea vya mbu kwenye madimbwi hayo
• Ondoa vitu vyote vinavyoweza kuweka mazalio ya mbu kama vile, vifuu vya nazi,makopo nk.
• Fyeka vichaka vilivyo karibu na makazi ya watu
• Funika mashimo ya maji taka kwa mfuniko imara
• Kujikinga na kuumwa na mbu
• Tumia dawa za kufukuza mbu“mosquito repellants”
• Vaa nguo ndefu
• Tumia vyandarua vilivyotibiwa
• Weka wavu kwenye madirisha na milango ya nyumba za kuishi
Hatua zinazochukuliwa na Wizara ya Afya na ustawi wa jamii
Kutoa taarifa ya kuwepo kwa ugonjwa katika ofisi za Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na Zanzibar
Kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa ugonjwa huu katika mkoa wa Dar es salaam na Zanzibar
• Watumishi wa afya wa wilaya zote 3
za Dar es salaam wamepewa mafunzo ya ziada ya namna ya kutambua,kutibu
na kuthibitisha ugonjwa huu
• Kuanzishwa kwa vituo maalum vya
ufuatiliaji wa ugonjwa huu katika hospitali 3 za wilaya za Dar es salaam
na hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar
Kuimarisha Utambuzi wa ugonjwa katika maabara ya NIMR, Dar es salaam
• Wizara imeshapatiwa msaada na CDC wa vitendanishi(Primers na Probes) ili kuweza kuthibitisha ugonjwa huu
Kuimarisha Uwepo wa ugonjwa huu katika mbu
Wizara kwa kushirikiana na NIMR itafanya utafiti wa kuwepo kwa virusi vya ugonjwa huu katika mbu aina ya Aedes Aegypt
Wananchi wanashauriwa kutokuwa na
hofu kwani mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyekwisha kufariki. Vile
vile wanashauriwa kutoa taarifa kwenye kituo cha huduma za afya kilicho
karibu mara watakapoona mgonjwa yeyote atakayehisiwa kuwa na dalili za
ugonjwa huu.
|
0 MAONI :
Post a Comment