Tangaza na Abd Da Hustler

Moto wa Rais Magufuli umeendelea bandarini, wengine wamesimamishwa leo..

Moto wa Rais Magufuli umeendelea bandarini, wengine wamesimamishwa leo..



Mpaka leo hii December 07 2015 tunahesabu kama mwezi mmoja hivi umepita tangu Rais Magufuli aapishwe na aanze kazi ya Urais wa awamu ya tano Tanzania.

Mfululizo wa stori zenye uzito wa kasi yake kwenye Urais zimekuwa zikitufikia kila siku, ya leo bado inabeba headlines za bandarini kwa mara nyingine… tangu siku ya kwanza Waziri Mkuu Majaliwa Kassim amefanya ziara ya ghafla bandarini mengi yameripotiwa ikiwemo ishu ya ubadhirifu, rushwa, kukwepa kodi ya upotevu wa makontena.

Mpya iliyonifikia kutoka bandarini inahusu kutenguliwa kwa uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi wa bandari, Awadhi Massawe, na pia kuvunja bodi ya bandari Dar es Salaam.

Kingine ni kwamba Rais Magufuli pia amemsimamisha kazi Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Shabani Mwanjaka.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment