Tangaza na Abd Da Hustler

FAHAMU UKWELI KUHUSU MAGONJWA YA ZINAA.

Kuna takribani magonjwa 25 ya zinaa ambayo kila mojawapo huwa na dalili zake tofauti na lingine, watu huambukizana bila kujua, isipokuwa kwa mtu mwenyewe kujitambua kuwa amekwisha ambukizwa.
Mara nyingi ugonjwa huu huambukizwa kwa kwa kufanya mapenzi bila kinga, kunyonyana ndimi (denda) na kushika shika nyeti. Ugonjwa huu huenea kimia kimia kwa wingi siku hizi, kutokana na watu kutokuwa na elimu kuhusu ugonjwa huu. Hapa unaweza kuona ukweli na uwazi kuhusu ugonjwa huu, nahivyo utaweza kujikinga au kuwahi hospitali kupata tiba mbadala.

Kwanza, Ugonjwa wa zinaa ambao kitaalamu hufahamiaka kama sexul transmitted disease (STD) ni ugojwa ambao huambukizana watu wanapokuwa wanafanya tendo la ngono linalokutanisha nyeti zao au kufanya mapenzi kwa aina yoyote ile kama kunyonyana ndimi.Pia magonjwa kama HIV/AIDS huambukizwa kwa kuchangia sindano na vitu vingine vyenye ncha kali.

Pili, Kama mtu amekwisha ambukizwa ugonjwa wa zinaa na bado hajaona madhara au dalili yoyote ya ugonjwa huo, bado akifanya mapenzi na mpenzi wake bila kutumia kinga, anaweza kumuambukiza ugonjwa huo mpenzi wake. Hata hivyo kwa ujumla watu hawawezi kutambua kama wameambukizwa ugonjwa huu kama hawajaona dalili zozote za ugonjwa huo.Unashauriwa endapo utakuwa na mashaka kuwa umeambukizwa, nenda haraka katika kituo cha afya kilichopo jirani yako ukapimwe na uanze kutumia dawa utapona kabla ya kupata madhara makubwa.

Tatu, Njia pekee ya kuepuka kupata maambukizi na madhra ya ugonjwa huu wa zinaa, ni kutofanya mapenzi na mwanamke au mwanaume mwenye ugonjwa huu au kutumia kondom.Kuna aina mbali mbali za kondom ambazopatikana katika madukani, kwa mfano kuna kondom za kike na za kiume. Kumbuka kuwa vidonge vya mpango wa uzazi vinaweza kuzuia kupata mimba tu, havizuii kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Ushauri wa mwisho, kama umekwisha ambukizwa ugonjwa huu na umepata maelekezo ya kutumia dawa na daktari, basi hakikisha unamaliza dozi yote na kuwa karibu na dokta kwa matibabu ya ziada.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment