
KUFUATIA Mwezi Mtukufu wa Ramadhani,
staa wa Filamu za Kibongo, Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ au maarufu
kama Madam amebadilika na kuondoa vitu vyote visivyo vya asili mwilini
mwake.
Wema alitupia picha yake kwenye
mtandao wa kijamii akionekana amekata nywele zote huku akiwa ameondoa
kope za bandia na kutoa kucha alizobandika kuashiria kuuheshimu mwezi
huu huku akibaki na kila kitu cha asili yake.
“Mwezi Mtukufu ni wa kuheshimiwa na
kuweka kila kitu pembeni, nafurahi kuwa hivi kwa maana hata kama
nikifunga swala zangu zitapokelewa vizuri,” alisema Wema
0 MAONI :
Post a Comment