Tangaza na Abd Da Hustler

Njama ya uasi yatibuka Ivory Coast

                                          Gereza la Maca ambako wahalifu sugu wanafungwa
Njama ya uasi pamoja na jaribio la wafungwa kutoroka jela kubwa zaidi nchini Ivory Coast imetibuka na kusababisha vifo vya wafungwa wawili.
Polisi walilazimika kurusha gesi ya kutoa machozi pamoja na kufyatua risasi ili kutuliza hali katika gereza la Maca mjini Abidjan.
Maafisa wanasema kuwa walinzi wawili wa magereza walijeruhiwa vibaya.
Purukushani lilizuka Jumanne jioni wakati wafungwa kadhaa walipovunja milango ya magereza yao na kuwaachilia huru baadhi ya wafungwa.
Gereza hilo huwahifadhi wahalifu sugu na baadhi ya maafisa kutoka kwa iliyokuwa serikali ya rais wa zamani Laurent Gbagbo.

Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment