Sylvia ni msichana wa miaka minane anaishi kijiji kimoja Tanzania, licha
ya maisha yake amejitolea kupata elimu na kila siku hutembea kwa saa
moja unusu kwenda shuleni. Yeye ni miongoni mwa wasichana waliobahatika
kupata elimu Barani Afrika
Mamake Sylvia aliolewa tena baada ya mumewe wa kwanza na babake Sylvia
kufariki dunia. Familia
hii inaishi kilomita 300 kutoka Jiji Kuu Dar Es
Salaam.
Shule ya Sylvia iko kilomita saba na msichana huku hutembea kila siku
akipitia kichakani,wakati mwingine anaumia miguu, pia lazima aepuke
kukanyanga wanyama hatari kama nyoka.
Mtoto huyu hupitia njia nyingi familia yake ni masikini na haiwezi
kumnunulia viatu. Japo hakuna karo anayolipiwa, imekua vigumu kwa wazazi
wake kununua vitabu au sare za Sylvia za shule.
Safari ya msichana huyu kisha inampeleka barabara kuu. Wakati mwingine
kuna jua kali, vumbi nyingi. Msimu wa jua barabara hujaa mapote na
inampa changamoto msichana huyu katika safari yake shuleni
Ikiwa msichana huyu hataki vumbi na matope ya barabara, huamua kupitia
kwenye njia ya reli. Hata hivyo kuna hatari zake, treni huenda
ikaamkanyanga. Wakati mwingine watoto wa shule wamekua wakitekwa nyara.
Kuna vichochoro vingine kando ya barabara kuu ambavyo Sylvia hutumia, lakini kuna hatari ya kukumbana na wabakaji.
Baada ya pita pita hizo hatimae Sylvia huwasili shuleni.Msichana huyu
anasema ataendelea na elimu yake licha ya safari ndefu ambayo hufanya
kila siku.
Sylvia ana rafiki Radhia ambaye huandamana naye kuelekea shuleni pamoja.
Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu na Utawaduni-UNESCO
asili mia 62 ya wasichana Afrika wameweza kuingia shule za upili, hata
hivyo nchini Tanzania ni asili mia 32 pekee ya wasichana ambao wanaweza
kujiunga na shule za upili.
BBaba wa kambo wa Sylvia amekua akiona malezi yake kama mzigo hasa elimu,
lakini kwake Sylvia anasema elimu ni njia pekee ya kubadilisha maisha
ya familia yake.
MWISHO;
Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
0 MAONI :
Post a Comment