Tangaza na Abd Da Hustler

Iran, Pakistan na Saudia zaongoza kwa kunyonga

Ongezeko la idadi ya watu wanaonyongwa ulimwenguni lilisababisha watu zaidi kuuawa kwa njia hiyo mwaka uliopita ikilinganishwa na kipindi chochote tangu mwaka 1989,shirika la haki za kibibaadamu la Amnesty International limesema.

Takriban watu 1634 walinyongwa mwaka 2015,ikiwa ni ongezeko la asilimia 50 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Iran,Pakistan na Saudia Arabia walihusika na asilimia 89 ya watu wote walionyongwa duniani.
Amnesty International

Jumla hiyo haishirikishi China ambapo Amnesty International imesema kuwa maelfu zaidi waliuawa lakini rekodi zake zikafichwa.

Kwa upande mwengine,kundi hilo limesema kuwa kwa mara ya kwanza mataifa mengi duniani yalifutilia mbali hukumu ya kunyonga.

Mataifa ya Fiji,Madagascar ,Congo Brazaville na Suriname yalibadilisha sheria zao mwaka 2015,huku Mongolia ikipitisha sheria mpya itakayoanza kutekelezwa baadaye mwaka huu.

Vifaa vinavyotumiwa na serikali ya China kuwashinikiza watu kukubali makosa

Amnesty imesema kuwa China bado inaongoza miongoni mwa mataifa yanayonyonga watu.Inakadiriwa kwamba maelfu ya watu walinyongwa huku maelfu ya wengine wakipewa hukumu ya kunyongwa mwaka 2015.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment