Umoja wa mataifa unasema kuwa kiongozi mmoja mkuu wa
kundi la wapiganaji wa kiisilamu nchini Somalia, al-Shabab, Hassan Dahir
Aweyes, amejisalimisha kwa wanajeshi wa Somalia.
Bwana Aweyes alitafuta hifadhi mjini Adado,mji
ulio umbali wa kilomita miatano kaskazini mwa Mogadishu baada ya
mapigano makali kati ya mirengo ya Al Shabaab mwishoni mwa wiki.Viongozi wa kiukoo, wamekwenda huko kujadili watakachofanya naye baada ya kujisalimisha kwake.
Lakini viongozi hao wamefahamisha mwandishi wa BBC kuwa amekanusha madai kuwa amejisalimisha na kwamba amekataa kusafiri kwenda Mogadishu.
Bwana Aweyes amekuwa akijulikana kama kiongozi mkubwa katika kundi la al-Shabab na Umoja wa mataifa na Marekani zinamfahamu kama gaid

0 MAONI :
Post a Comment