Tangaza na Abd Da Hustler

Maelfu ya watu wanakimbilia usalama wao kutokana na vita kutokota Sudan Kusini


Maelfu ya watu wanakimbilia usalama wao kutokana na vita kutokota Sudan Kusini
Ripoti kutoka Sudan Kusini zinasema kuwa wanajeshi walio watiifu kwa serikali ya rais Salva Kiir wanaendelea kuukaribia mji wa Bentiu unaodhibitiwa na waasi katika eneo lenye utajiri wa mafuta Kaskazini mwa taifa hilo.
Mwandishi wa BBC aliye mjini Bentiu anasema wanajeshi wa serikali wanaaminika kuwa umbali wa kilomita ishirini na tano kutoka mji huo na raia wameingiwa na hofu kubwa.
Maelfu ya watu wanaripotiwa kukimbilia kwenye makao ya jeshi la kulinda amani ya umoja wa mataifa katika mji huo.
Wanajeshi wanaomtii aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar wameripotiwa kuanza kujiondoa katika eneo la makabiliano.
Mapigano yaliyozuka kote nchini Sudan kusini mwezi uliopita na ni mafanikio kidogo yaliyofikiwa katika mazungumzo ya kumaliza ghasia hizo
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment