Mtayarishaji ameiambia Hollywood Reporter kuwa filamu hiyo haitaumiza hisia za ndugu na jamaa za abiria waliopotea na ndege hiyo na kwamba hakuna matumizi yoyote ya bunduki yatakayooneshwa.
“Haitahusu vitu vya kijinga. Hakutakuwa na matumizi ya bunduki na hakutakuwa na matumizi mabaya ya vitu vya kigeni.” Alisema Rupesh Paul.
Katika kutetea uamuzi wake wa kutumia tukio hilo kama sehemu ya filamu yake, alieleza kuwa haoni umuhimu wa kutengeneza filamu ambayo haiwavutii watu.
“Watu hawataki Makala, wanataka kitu kitakachowasisimua. Kwa nini nitayarishe filamu kuhusu kitu kingine chochote ambacho hakiwavutii watu?” Alihoji.
0 MAONI :
Post a Comment