Tangaza na Abd Da Hustler

Diamond kurekodi wimbo na Mafikizolo

Leo ni siku ambayo mashabiki wa muziki Afrika na duniani wataiangalia Durban kwa macho mawili au kusikiliza kinachoendelea huko kwa masikio yote kwa kuwa MTV MAMA zitatolewa usiku.
Diamond Platinumz ambaye ni mwakilishi wa Tanzania pekee anaeshindania tuzo hizo, anazidi kuongeza connections na kujitanua zaidi wakati akisubiria utoaji wa tuzo hizo.
Katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jana kwa ajili ya MTV MAMA , kundi la Mafikizolo kutoka Afrika Kusini lilithibitisha kuwa linafanya mazungumzo nae kuhusu kushirikishana kwenye wimbo.
Diamond anawania tuzo katika vipengele viwili. Msanii bora wa kiume, na wimbo bora wa kushirikishana (Number One Remix aliofanya na Davido).
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment