Tangaza na Abd Da Hustler

Uchaguzi mkuu wafnyika Syria

Uchaguzi mkuu wafanyika Syria wapiga kura wakisema wanaumuunga mkono Rais Asaad
Taifa la Syria linafanya uchaguzi mkuu ambao upinzani umepuuza. Rais Bashar al-Assad anatarajiwa kupata ushindi kwa urahisi dhidi ya wapinzani wake wawili walioidhinishwa na serikali .
Upinzani unaoungwa mkono na mataifa ya magharibi umepinga uchaguzi huo na kuususia huo .
Kwa mara ya kwanza katika miaka hamsini, familia ya Assad inakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa wagombea wawili, lakini Rais Bashar al-Assad, ambaye ashapiga kura na mkewe Asmaa, anatarajiwa kushinda uchaguzi huo.
Wakazi wa Damascus wameambia BBC kuwa wanampigia kura Rais Assad kwa sababu anapambana dhidi ya tisho la ugaidi.
Katika maeneo ambayo hana udhubiti, uchaguzi haufanyiki.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa ingawa kila mtu ambaye ameongea naye anaunga mkono Assad, serikali imechukulia uchaguzi huu kwa uzioto huku ikiwasafirisha wapiga kura kwa mabasi kupiga kura.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment