Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa leo imepokea taarifa
kutoka Ubalozi wa Libya hapa nchini kuwa aliyekuwa Kaimu Balozi wa
Libya, Bwana Ismail Nwairat, amefariki dunia jana kwa kujipiga risasi.
Taarifa hiyo ya ubalozi imeeleza kuwa kifo hicho kimetokea majira ya saa
Saba mchana ofisini kwa Kaimu Balozi huyo katika jengo la Ubalozi wa
Lbya. Inataarifiwa kuwa Bwana Nwairat alijifungia ofisini na
kujifyatulia risasi kifuani upande wa kushoto. Maafisa ubalozi walivunja
mlango waliposikia mlipuko wa bunduki na kumkuta Kaimu Balozi Nwairat
ameanguka chini. Walimkimbiza hospitali ya AMI Oysterbay ambako
alitangazwa kuwa alikwisha kufariki na Polisi walithibitisha kifo hicho.
Maiti imehamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili. Ubalozi unafanya
maandalizi ya kusafirisha…
0 MAONI :
Post a Comment