Tangaza na Abd Da Hustler

Rihanna ampigia mikausho Chris Brown kwenye mechi ya basketball

.

0
Chris Brown na Rihanna wamejikuta wapo karibu kwa umbali mdogo sana walipokua kwenye mechi ya basketball kwa ajili ya kuchangia taasisi ya CC Sabathia na Robinson Cano. Mechi hiyo ilikuwa ya mafanikio kwa kuingiza zaidi ya dola milioni 1 lakini story kubwa sio hiyo.
Kitu kilichotengeneza headline ni pale Rihanna alivyoonyesha mikausho mikali hasa wakati Chris Brown anapokuwa karibu yake wakati wa mechi hiyo. Kuna wakati Chris Brown alikuwa anawasalimia mashabiki waliokuwa wamekaa karibu na kiti cha Rihanna na picha zilipigwa Rihanna anaonekana ameweka mikausho na kuangalia pembeni.
Mechi iliisha vizuri na picha ya hapo juu imekuwa maarufu sana kwenye instagram hivi sasa.
1
2
3
4
5
6
7
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment