Tangaza na Abd Da Hustler

LA LIGA: REAL MADRID YAFUNGA MWAKA KWA REKODI MPYA, RONALDO JUU!

Real Madrid Jana wamepata ushindi wao wa 20 mfululizo katika Mashindano yote huku Cristiano Ronaldo akipiga Bao 2 wakati walipoifunga Ugenini Almeria Bao 4-1 katika Mechi ya La Liga.

Real wameshinda Mechi zao zote kuanzia Septemba 13 na wapo Mechi 4 nyuma ya Rekodi ya Dunia ya kushinda Mechi 24 mfululizo iliyowekwa na Klabu ya Brazil Coritiba Mwaka 2011.

Hadi Mapumziko, Real walikuwa mbele kwa Bao 2-1 kwa Bao za Isco na Gareth Bale

Kwenye Mechi hiyo, Kipa Iker Casillas aliokoa Penati iliyopigwa na Verza.

Kipindi cha Pili Real walipiga Bao 2 nyingine kupitia Ronaldo na kushinda Bao 4-1.

Hivi sasa Ronaldo amefunga Jumla ya Mabao 32 kati Mechi 23 na kwenye La Liga ana Bao 25 katika Mechi 14.

++++++++++++++++++++++++

MAGOLI:

Almería1

-García Rabasco 39′

Real Madrid4

-Isco 34′

-Bale 42′

-Ronaldo 81′ & 88′

++++++++++++++++++++++++

Juzi Jumanne, Real walivunja Rekodi ya Barcelona ya kushinda Mechi 18 mfululizo walipoifunga Lugorets kwenye Mechi yao ya mwisho ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Mechi hii ya La Liga na Almeria ni ya mwisho kwa Real kwa Mwaka huu kwa vile wao wanasafiri kwenda Nchini Morocco kucheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu yaliyoanza Desemba 10 na wao wakiwa Wawakilishi wa Ulaya kama Klabu Bingwa.

wamebeba Makombe ya UEFA CHAMPIONZ LIGI na Copa del Rey.

Hivi sasa Real wapo Pointi 5 mbele ya Barcelona kwenye La Liga.

VIKOSI:

Almeria (Mfumo 4-2-3-1): Ruben; Michel, Navarro, Trujillo, Velez; Teye, Verza; Mendez, Soriano, Dubarbier; Hemed

Akiba: Julian, Dos Santos, Corona, Azeez, Zongo, Mane, Wellington, Bifouma.

Real Madrid (Mfumo 4-3-3): Casillas; Carvajal, Pepe, Varane, Marcelo; Illarramendi, Kroos, Isco; Bale, Benzema, Ronaldo.

Akiba: Navas, Arbeloa, Coentrao, Medran, Nacho, Jese, Chicharito.

LA LIGA

RATIBA

**Saa za Bongo

Ijumaa Desemba 12

UD Almeria 1 Real Madrid CF 4    

Jumamosi Desemba 13

18:00 Getafe CF v FC Barcelona  

20:00 Valencia C.F v Rayo Vallecano     

22:00 Cordoba CF v          Levante      

Jumapili Desemba 14       

0:00   Malaga CF v Celta de Vigo

14:00 RCD Espanyol v Granada CF       

19:00 Sevilla FC v SD Eibar        

21:00 Atletico de Madrid v Villarreal CF 

23:00 Real Sociedad v Athletic de Bilbao         

Jumatatu Desemba 15

22:45 Deportivo La Coruna v Elche CF  

Ijumaa Desemba 19

22:45 Celta de Vigo          v UD Almeria

Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment