Tangaza na Abd Da Hustler

Boko Haram 800 wajisalimisha Nigeria


Wapiganaji 800 wa kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram wamejisalimisha kwa Jeshi la Nigeria.

Wapiganaji 800 wa kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram wamejisalimisha kwa jeshi la Nigeria.

Hatua hiyo inafuatia mpango mahsusi wa 'Operation Safe Corridor' unaolenga kuwapokea wapiganaji wa kundi hilo la kigaidi ambalo limesababisha vifo vya maelfu ya raia wa Nigeria.

Chini ya mpango huo wapiganaji wanaojisalimisha wanachukuliwa na kufunzwa upya njia mbadala ya kujitafutia riziki.


Msemaji wa jeshi amesema kuwa wanania ya kuwasamehe wapiganaji wa Boko Haram watakaotubu makosa yao.

Msemaji wa jeshi amesema kuwa wanania ya kuwasamehe wapiganaji wa Boko Haram watakaotubu makosa yao.

Kwa sasa wamewekwa kwenye makazi maalum ambapo wanaendelea kupata mafunzo ya msimamo wastani wa kidini.


Wakaazi milioni moja wanaishi katika kambi za wakimbizi wa ndani kwa ndani

Baadaye watafunzwa mbinu mpya za kujitafutia riziki kabla ya kupewa mtaji wa kuanza upya maisha yao.

Hata hivyo kuna hofu iwapo jamii itakuwa tayari kuwapokea wapiganaji waliotekeleza maasi dhidi yao.


Zaidi ya watu 10,000 waliuawa huku takriban wakaazi milioni moja wakitoroka makwao tangu uasi huo uanze yapata miaka 7 iliyopita.

Wahanga wa maasi yao ndio wanaotarajiwa kuwa na wakati mgumu zaidi kuwapokea ama hata kuwasamehe wapiganaji hao wa zamani.

Eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria ndilo lililoathirika sana na mashambulizi ya Boko Haram.

Zaidi ya watu 10,000 waliuawa huku takriban wakaazi milioni moja wakitoroka makwao tangu uasi huo uanze yapata miaka 7 iliyopita.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment