Uongozi wa klabu ya Dar Es Salaam Young Africans leo April 6 kupitia kwa afisa habari wake Jerry Muro ameongea na vyombo vya habari na kuelezea taarifa za mchezo wao wa klabu Bingwa barani Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri utakaochezwa April 9 2016 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.
Jerry amethibitisha Al Ahly kuwasili Dar Es Salaam alfajiri ya leo, pamoja na CAF kutoa majina ya waamuzi wa mchezo huo ambao wanatoka Ivory Coast Denis Dembele, Mauris Donatien, Moussa Bayere, Tangba Kambou lakini kamisaa wa mchezo Celestine Ntangungira anatokea Rwanda.
Jerry Muro
Hadi sasa Yanga mechi zao zilizopita za klabu Bingwa Afrika waligoma zisioneshwe kwenye TV ” Kwa sasa viongozi wanafanya utaratibu wa kuangalia namna ambavyo tunaweza kuruhusu TV kuonesha mchezo huo, lakini watu wajue tutaruhusu matangazo ya TV yarushwe mikoani kasoro Dar na Pwania ndio maana tumeweka kiingilio cha chini elfu tano” >>> Jerry Muro
KAMA ULIKOSA KUTAZAMA VIDEO YA MAGOLI YA YANGA VS KAGERA SUGAR APRIL 3 2016
Home
/
HABARI
/
MICHEZO
/
Kwa wanaosubiri mchezo wa Yanga Vs Al Ahly ya Misri, kuna taarifa mpya hapa
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 MAONI :
Post a Comment