Tangaza na Abd Da Hustler

Muda wa kupiga kura waongezwa Iran

Televisheni ya taifa ya Iran imesema kwamba vituo vya kupigia kura vitakuwa wazi kwa saa mbili zaidi kutokana na kujitokeza kwa idadi kubwa ya watu wanaotaka kupiga kura.
Imesema kwamba kutokana na watu kujitokeza kwa wingi maafisa wa uchaguzi wameomba kuongezwa muda kwa saa mbili hadi hapo saa kumi na moja na nusu jioni na kwamba waziri wa mambo ya ndani Mostafa Mohammad Najjar amelikubali ombi hilo. Baraza la Walezi  linaloangalia uchaguzi huo limesema hakukuwa na matatizo yoyote . Wizara ya mambo ya ndani haikutowa takwimu zozote zile juu ya idadi ya watu waliojitokeza kupiga kura lakini kwa mujibu wa waandishi wa habari wa AFP baadhi ya vituo vya kupigia kura katika mji mkuu wa nchi hiyo vilikuwa vimefurika wapiga kura.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment