Tangaza na Abd Da Hustler

Obama kukutana na mpizani wa Merkel

Rais Barack Obama wa Marekani pia atakutana na mpinzani mkuu wa Kansela Angela Merkel katika uchaguzi mkuu ujao mbali na Kansela mwenyewe na rais wa Ujerumani Joachim Gauck wakati wa ziara yake  nchini Ujerumani wiki ijayo.
Kwa mujibu wa taarifa ya serikali Obama ambaye anatarajiwa kuwasili katika mji mkuu wa Ujerumani Jumanne usiku akiandamana na mke wake Michelle baada ya kuhudhuria Mkutano wa Kilele wa Kundi la Mataifa Manane Tajiri duniani huko Ireland ya Kaskazini atakutana na Peer Steinbruck mgombea wa ukansela wa chama cha upinzani cha siasa za wastani za mrengo wa shoto  Social Demokratik SPD
Ikiwa ni miezi mitatu kabla ya uchaguzi  mkuu hapa nchini .
Merkel atampokea Obamba Jumatano asubuhi katika ofisi ya kansela na baadae watakuwa na mkutano wa pamoja na waandishi wa habari.
Syria,Afghanistan na Mashariki ya kati,mpango wa nuklea wa Iran na mpango wa upelelezi wa mtandao wa Marekani uliofichuliwa hivi karibuni yatakuwa ni miongoni mwa agenda ya mkutano wao.
  
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment