Msemaji wa jeshi la Mali Luteni Kanali Souleymane Maiga, amesema kwa
mara ya kwanza wanajeshi wameingia mji wa Kidal ulioko kaskazini mwa nchi
hiyo tangu walipoondolewa miezi 16 iliopita na waasi wa Tuareg na baadaye
na jeshi lililokuwa na mafungamano na kundi la kigaidi la Al Qaida.
Mji wa Kidal kama maeneo mengine kaskazini mwa Mali uliingia katika mikono mbali mbali ya waasi tangu mwezi Machi mwaka jana. Msemaji huyo wa jeshi amesema jeshi liliingia Kidal saa kumi na moja jioni hapo jana na kuelekea hadi katika kambi ya kwanza ya kijeshi mjini humo.
Wanajeshi hao waliandamana na wanajeshi wa Ufaransa kama walivyofanya walipoikomboa miji ya Gao na Timbuktu mwezi wa Januari mwaka huu.
Mji wa Kidal hapo awali ulikuwa unatawaliwa na waasi wa Kituareg ambao sasa wametia saini makubaliano na serikali ya Mali, kuliwezesha jeshi hilo kurudi tena mjini humo.
Mji wa Kidal kama maeneo mengine kaskazini mwa Mali uliingia katika mikono mbali mbali ya waasi tangu mwezi Machi mwaka jana. Msemaji huyo wa jeshi amesema jeshi liliingia Kidal saa kumi na moja jioni hapo jana na kuelekea hadi katika kambi ya kwanza ya kijeshi mjini humo.
Wanajeshi hao waliandamana na wanajeshi wa Ufaransa kama walivyofanya walipoikomboa miji ya Gao na Timbuktu mwezi wa Januari mwaka huu.
Mji wa Kidal hapo awali ulikuwa unatawaliwa na waasi wa Kituareg ambao sasa wametia saini makubaliano na serikali ya Mali, kuliwezesha jeshi hilo kurudi tena mjini humo.
About Unknown
Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
0 MAONI :
Post a Comment