Tangaza na Abd Da Hustler

Umoja wa Afrika walaani mapinduzi Misri

Umoja wa Africa umelaani hatua ya jeshi la Misri kumpindua Rais Mohammed Mursi. Sasa Umoja huo umeusimamisha uanachama wa nchi hiyo, huku ikitaka hali ya kikatiba irudishwe nchini humo na kuikumbusha Misri juu ya msimamo wake thabiti dhidi ya mabadiliko yanayoenda kinyume na katiba
Katika mkutano wa Baraza la amani na usalama la Umoja wa  Afrika uliofanyika hapo  jana kwenye makao yake makuu mjini Adis Ababa, Ethiopia, Umoja huo pia umesema kuondolewa madarakani  kwa Mohammed Mursi maana yake ni kuchukuliwa kwa  mamlaka na jeshi kinyume na sheria.

Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment