Tangaza na Abd Da Hustler

Tazama Video.. Udugu wa kiislamu Misri waapa kupambana

Udugu wa kiislamu umeitisha maandamano nchini Misri leo kwa kughadhabishwa na kung'olewa madarakani na jeshi kwa Rais Mohammed Mursi na kukamatwa kwa kiongozi wao na maafisa wengine wakuu.Kuna hofu kuwa kuondolewa madarakani kwa Mursi huenda kukazua ghasia nchini humo na makundi ya zamani ya wapiganaji wenye itikadi kali yameapa kupigana.Wapiganaji wa kiislamu wanashukiwa kuyashambulia maeneo manne  kaskazini mwa Sinai wakilenga vituo viwili vya ukaguzi vya kijeshi,kituo cha polisi na uwanja wa ndege wa el Arish ambako kuna ndege za kijeshi.Mwanajeshi mmoja aliuawa na wengine watatu kujeruhiwa kulingana na maafisa wa usalama ambao hawakutaka majina yao kutajwa kwasababu hawana ruhusa ya kuzungumza na wanahabari.Chama hicho kilipigwa marufuku kwa miaka mingi nchini Misri  hadi alipong'olewa madarakani  Rais Husni Mubarak. Mursi ndiye Rais wa kwanza kuchaguliwa na wamsri kutoka  chama cha udugu wa kiislamu.Uchaguzi huo pia ulikuwa wa kwanza wa kidemokrasia  nchini humo. 

Muslim Brotherhood wito kwa wingi mikutano ya kampeni ya kusaidia Mohamed Morsy. CNN Ian Lee ripoti

Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment