Tangaza na Abd Da Hustler

Syria kuheshimu mikataba yake iliyosaini

Rais wa Syria, Bashar al-Assad amesema hana wasiwasi na rasimu ya azimio lililowasilishwa na Marekani, Ufaransa na Uingereza, kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Kituo cha televisheni cha China CCTV, kimeripoti leo kuwa Assad amesema tangu Syria ipate uhuru wake, nchi hiyo imekuwa ikizingatia mikataba yote iliyosaini. Amesema kuwa wataheshimu kila kitu walichokubaliana, akitolea mfano jinsi serikali yake ilivyokubali kusalimisha silaha zake za sumu chini ya udhibiti wa kimataifa. Amesema hatua ya kupelekwa kwa rasimu ya azimio hilo, au kuzitaka Marekani na Urusi kukubaliana kuhusu mpango wao, Marekani, Ufaransa na Uingereza zinajaribu kujionyesha kwamba zimeshinda vita dhidi ya Syria, nchi ambayo ni adui yao.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment