Idadi ya watu waliouawa katika shambulio la kujitoa muhanga katika Kanisa
nchini Pakistan, imefikia 81, huku Wakristu wakiandamana nchi nzima wakidai
ulinzi zaidi. Shambulio hilo la mabomu lililotokea kwenye Kanisa la Watakatifu
Wote, kaskazini-magharibi mwa mji wa Peshawar baada ya ibada ya Misa
jana Jumapili, linaaminika kuwa baya kabisa dhidi ya jamii ya Wakristu walio
wachache. Dokta Arshad Javed, amesema watu wengine 131 wamejeruhiwa
katika shambulio hilo. Paul Bhatti, rais wa muungano wa jamii za watu
wachache nchini Pakistan, amesema wanaamini kuwa shambulio hilo ni
kitendo cha kigaidi. Bhatti ambaye aliwahi kuwa waziri wa maelewano ya
kitaifa katika serikali iliyopita, amesema Wakristu sio walengwa pekee wa
ugaidi, bali nchi nzima inaathirika na ugaidi.
Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
0 MAONI :
Post a Comment