Janjaro msanii
kutoka Arusha lakini makazi yake yapo Dar amefunguka na DJCHOKAblog kuwa
hajafukuza na Ostaz Juma Namusoma kwenye kampuni yake ya Mtanashati
bali amejitoa mwenyewe kwa hiari yake. Janjaro amesema amechoka na
matendo tu ya Ostaz na alikuwa tu akiyavumilia lakini kwa sasa
ameshakuwa mkubwa so nataka nikae kivyangu vyangu nifanye mambo yangu
kama wasanii wengine ambao hawana meneja na wanafanya poa. Namnukuu
Janjaro akisema....
"Najua yatasemwa mengi
kutoka kwa Ostaz Juma ila mimi ndio uwamuzi wangu, kuna watu wanasema
sina utovu wa nidhamu lakini hao watakuwa wananijua sasa hivi
hawajanifuatilia kutoka nyuma. Hata mtoto mdogo atakuwa mtundu ila akiwa
mkubwa hunyooka na kuwa mtoto mzuri sasa nimekuwa mkubwa na kupelekwa
pelekwa tena sitaki, kwa maelezo zaidi Ostaz Juma aongee na wazazi wangu
asiongee na mimi"
Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
0 MAONI :
Post a Comment