Marekani imetangaza kuiwekea vikwazo Rwanda na nchi nyengine kadhaa kwa kuhusika katika matumizi ya askari watoto jambo ambalo limekanushwa na Rwanda kuwa inawasaidia waasi wa M23 wenye kutumia askari watoto huko Congo.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Marie Harf amesema Rwanda inawekewa vikwazo hivyo kwa sababu ya kuliunga mkono kundi la waasi la M23 ambalo linaendelea kuwaandikisha watoto jeshini na kuwateka nyara na kwa hiyo kutishia utulivu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Kundi la M23 linalodhibitiwa na waasi wa Kitutsi ambao walikuwa wanajeshi wa zamani wa Congo walianza kuteka sehemu za mashariki ya Congo hapo mwaka jana kwa kuituhumu serikali kwa kushindwa kutimiza makubaliano yao ya amani ya mwaka 2009.
Harf amesema Rwanda haitopatiwa msaada wa kifedha wa kijeshi wa kimataifa kutoka Marekani kusaidia masuala ya elimu na mafunzo jeshini. Pia haitopatiwa msaada wa kugharamia majeshi ya kigeni unaohusu mauzo ya zana za kijeshi za Marekani na huduma za kijeshi.
Yapinga kuwajibishwa na matukio ya Congo
Kundi la waasi wa M23 wakiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani vikwazo hivyo pia vimewekwa kwa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Myanmar,Sudan na Syria lakini haiko wazi iwapo nchi hizo zinapata msaada wa kijeshi wa Marekani.
Lengo kukomesha matumizi ya askari watoto
Askari mtoto akiwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Nchi nyengine tatu ambapo majeshi yao yanajulikana kwa kuwaandikisha na kuwatumia askari watoto ambazo ni Chad, Sudan Kusini na Yemen zimeondolewa vikwazo vya kijeshi vya Marekani kwa mujibu wa afisa mwandamizi wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani aliyezungumza kwa masharti ya kutotajwa jina lake.Na kwa ajili ya maslahi ya Marekani, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Somalia zimeondolewa kwa kiasi fulani vikwazo hivyo vya kijeshi.
0 MAONI :
Post a Comment