Ujumbe wa wataalamu wa kuziondoa silaha
za sumu umewasili nchini Syria kuanza
jukumu la kuziorodhesha silaha hizo ili
kuziteketeza hapo baadae.
Wakaguzi hao kutoka shirika la kimataifa la
kudhibiti silaha za sumu lenye makao mjini
The Hague, OPCW waliwasili Syria kwa
magari kutokea Lebanon, siku moja baada ya
wataalamu wa Umoja wa Mataifa, waliokuwa
wanafanya uchunguzi juu ya madai ya
kutumika silaha za sumu, kuondoka nchini
Syria.
Wakaguzi hao wa shirika la OPCW wapo
Syria kulitekeleza azimio la Umoja wa Mataifa
linaloitaka Syria iziteketeze silaha zake za
sumu hadi ifikapo kati kati ya mwaka ujao.
Syria inasemekana kuwa na tani zaidi ya alfu
moja ya gesi za sarin na mustard na silaha za
sumu za aina nyingine zilizopigwa marufuku.
Silaha hizo zimewekwa katika sehemu 45
tofauti nchini Syria kote.
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 MAONI :
Post a Comment