Aliekuwa Waziri Mkuu wa Italia Silvio
Berlusconi amegeukwa na wabunge kadhaa
wa chama chake kuhusu njama zake za
kutaka kuiangusha serikali ya mseto nchini
Italia wakati pana wasiwasi kwamba
mgogoro wa kisiasa katika nchi hiyo
inayoshika nafasi ya tatu kwa nguvu za
kiuchumi katika ukanda wa sarafu ya Euro
unaweza kusababisha athari duniani kote.
Waziri mkuu huyo wa zamani Berlusconi
alijitenga na serikali ya Waziri Mkuu wa sasa
wa Italia Enrico Letta, baada ya washirika wa
serikali ya mseto kukataa kuzuia taratibu za
kumfukuza Berlusconi bungeni kutokana na
mahakama kumtia hatiani kwa udanganyifu
wa kodi.
Berlusconi amepania katika mipango yake ya
kumwangusha Waziri Mkuu Enrico Letta
lakini anazidi kugeukwa na baadhi wabunge
wa chama chake ambao wamesema
wataiunga mkono serikali ya Waziri Mkuu
Letta.
Mpambe mwandamizi wa
Berlusconi,Angelino Alfano ambae ni waziri
wa mambo ya ndani amewaambia wabunge
wa chama cha Berlusconi-PDL, wamuunge
mkono Waziri Mkuu Letta kwa kumpigia kura
ya kuwa na imani nae leo bungeni.
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 MAONI :
Post a Comment