Tangaza na Abd Da Hustler

Waziri Mkuu Netanyahu ahutubia Umoja wa Mataifa

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amezitahadharisha nchi za magharibi juu ya Iran na  katika hotuba yake amezitaka nchi hizo zisimwamini rais mpya wa nchi hiyo.
Akihutubia kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa  Waziri Mkuu Netanyahu,pia alisema kwamba Israel   ipo tayari kuchukua hatua peke yake ili kuizuia Iran kuunda silaha za nyuklia.
Netanyahu aliwaambia wajumbe kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwamba yeye hamwamini Rais Hassan Rouhani wa Iran na kwamba mtu mwengine yeyote hapaswi kumwamini Rais huyo.
Amesema Rais Rouhani ni mbwa mwitu alievaa manyoya ya kondoo. Waziri Mkuu wa Israel aliitoa  hotuba hiyo siku moja tu baada ya kukutana na Rais   Obama kwenye Ikulu ya Marekani ambapo aliitaka Marekani iendelee kuishinikiza Iran.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment