Tangaza na Abd Da Hustler

Msumbiji: Hatuna washukiwa waliomuua Karegeya


Kareguya aliuawa nchini Afrika Kusini huku Rwanda ikisema alikuwa adui wake
Polisi nchini Msumbuji wamekanusha madai kuwa wamewakamata watu wanaoshukiwa kumuua mkuu wa zamani wa ujasusi nchini Rwanda Patrick Karegeya.
Msemaji wa polisi nchini humo Joao Machava amesema kuwa hakuna mshukiwa aliyezuiliwa kuhusiana na mauaji hayo ya Patrick Karegeya ingawa kuna raia kadhaa wa Rwanda waliokamatwa nchini humo.
Awali alinukuliwa akisema wanyarwanda kadhaa wamekamatwa na wanatarajiwa kurejeshwa nchini Afrika Kusini.
Marehemu Karegeya alikimbilia uhamishoni nchini Afrika Kusini na alipatikana akiwa amefariki katika hoteli yake mjini Johannesburg January tarehe moja.
Polisi wanaamini kuwa Karegeya aliuawa.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment