Katika hali ya kushangaza raisi wa klabu ya Zamalek ya
nchini Misri Mortada Mansour, ametangaza kufanya mazungumzo ya
kumsajili aliyewahi kuwa mchezaji bora wa dunia Ronaldo de Assis Moreira
*Ronaldinho Gaucho* ambae kwa sasa anaitumikia klabu ya Atlético
Mineiro ya nchini kwao Brazil.
Raisi wa Zamalek alitangaza mpango huo wakati akihojiwa kwenye kituo
cha televisheni cha taifa cha nchini Misri, ambapo amesema anaamini
watafanikiwa kukamilisha mpango wa kumsajili mshambuliaji huyo.
Hata hivyo mtangazaji Khaled Ghandour aliyekuwa anamuhoji Mortada
Mansour, alionyesha kushangazwa na taarifa hizo na kujikuta akiuliza
mara mbili mbili, lakini jibu aliloambulia kutoka kwa kingozi huyo
lilikuwa la kushangaza pia.
Mortada Mansour alirejesha swali kwa mtangazaji huyo kwa kumuuliza kwa
nini anashangazwa na taarifa hizo, ama anataka kuona wanamsajili Barack
Obama?
Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
0 MAONI :
Post a Comment