Mkutano
mkuu wa Chama cha wananchi CUF Taifa umewachagua tena Maalim Seif
Sharif Hamad kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho na Professa Ibrahimu
Lipumba kuwa mwenyekiti wa chama hicho, kwa kipindi cha miaka mitano
ijayo.
Kwa mujibu wa kura zilizopigwa, maalim Seif Sharif hamad amepata kura
675 za ndiyo, sawa na asilimia 99.5 ya kura zilizopigwa na Prof.
Ibrahim Lipumba amepata kura 659 sawa na asilimia 95.5 na kumshinda
mpinzani wake Chifu Lutalosa Yemba aliyepata kura 30 sawa na asilimia
4.3.
Source: EATV
0 MAONI :
Post a Comment