Tangaza na Abd Da Hustler

Victoria ya UG yashinda Cecafa Nile


Victoria iliicharaza AFC Leopards ya Kenya mabao 2-1
Timu ya Chuo Kikuu Cha Victoria kutoka Uganda imeibuka mshindi wa mashindano ya kandanda ya kombe la Cecafa Nile Basin yaliyomalizika Jumatano wiki hiimjini Khartoum, Sudan.
Victoria imeshangaza wengi kwa kutwaa kombe hilo baada ya kushinda AFC Leopards ya Kenya mabao 2-1 mjini Khartoum,Sudan.
Mabao mawili ya Victoria yalitulizwa kimyani na Odongo Matthew na Mutyaba Muzamir naye AFC Leopards ikapata bao moja la kuondoa aibu kupitia Ikene Austin.
Ilikua ni shangwe na hoi hoi kwa wachezaji wa Victoria kwani ni mwaka jana tu timu hiyo iliundwa ikilinganishwa na Leopards ambayo ilianzishwa mwaka wa 1964..
Victoria ilifuzu kushiriki mashindano hayo ya Sudan kwa kuibuka mshindi wa Uganda Cup, na katika ligi kuu ya Uganda ilimaliza ya pili..
Al Shandy ya Sudan ilimaliza ya tatu kwa kuicharaza Academie Tchite ya Burundi mabao 4-1 kwenye mechi ya kuamua mshindi wa tatu..
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment