Kwanza ni akaunti ya klabu yenye kitita cha Sh420 milioni, pili ni
Uwanja wa Bunju na tatu makubaliano yake na Benki ya Posta kuhusiana na
kadi za wanachama ambazo kama uongozi mpya utakuwa makini, klabu
itaingiza pesa nyingi kupitia mtindo huo.
Akikokotoa kiasi hicho cha Sh420 milioni, Rage alisema kati ya hizo
zimo Sh60 milioni za mauzo ya Shomari Kapombe aliyesajiliwa na Azam FC,
Sh160 milioni za kodi ya mapango ya jengo la Simba lililopo Kariakoo
jijini Dar es Salaam na Sh100 milioni za wadhamini.
Akizungumza na Mwanaspoti pia Rage alionyesha hisia zake juu ya kero
alizokuwa anakutana nazo alipokuwa madarakani, alisema: “Kuongoza klabu
kubwa kama Simba ni lazima ujitoe, hata hivyo vurugu kubwa za klabu
ambazo zinatokea huwa zinasababishwa na njaa tu. Hivyo kumaliza muda
wangu nashukuru maana nakwenda kupumzika.”
Source: Mwanaspoti
Source: Mwanaspoti
0 MAONI :
Post a Comment