Tangaza na Abd Da Hustler

Bunge la Ugiriki laidhinisha sheria ya kupunguza ajira

Bunge la Ugiriki limepiga kura kuunga mkono mswada wa sheria, unaohusu maandalizi ya kuzifuta nafasi 25,000 za ajira katika sekta ya umma. Sheria hiyo ni mojawapo ya masharti yaliyowekwa na wakopeshaji wa kimataifa, yaani Umoja wa Ulaya na Shirika la fedha ulimwenguni, IMF. Mswada huo ulipata wingi wa kura zilizohitajika kuuidhinisha, ambazo ni angalau 151 katika bunge lenye viti 300. Kura hiyo bungeni imepigwa muda mchache tu kabla ya ziara ya waziri wa fedha wa Ujerumani, Wolfgang Schäuble. Watu wanaopinga hatua hiyo walifanya maandamano kuupinga mswada huo. Waandamanaji walidai wanapigania haki ya tawala za mitaa na ile ya kuwapa watu nafasi ya kujiamulia mambo yao wenyewe.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment