Tangaza na Abd Da Hustler

UN kutazama upya ushirikiano wa kijeshi na Kinshasa

 Umoja wa Mataifa umesema unatazama upya msaada wake kwa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, baada ya ripoti kuwa jeshi hilo linawatesa mateka wa kundi la M23 lililowakamata, na kuzitendea maovu maiti za wale waliouawa. Jeshi la serikali ya Kongo lilitumia helikopta kuwashambulia waasi hao kwa siku tatu mfululizo, na maelfu ya wakaazi wamevihama vijiji vyao kuepuka mapigano. Makabiliano mapya baina ya jeshi la serikali na waasi wa M23 yaliibuka Jumapili iliyopita.
Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, imesema amehangaishwa na taarifa hizo. Aidha, katika taarifa hiyo, Ban aliitaka serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwafikisha mbele ya sheria wanajeshi waliohusika na uhalifu huo. Umoja wa Mataifa ulirejesha ushirikiano na jeshi hilo, baada ya kufikishwa mahakamani kwa maafisa wawili waliotuhumiwa kuwabaka wanawake katika eneo la Minova, mwezi Februari mwaka huu.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment