Raisi wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud
Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amenusurika
jaribio la kumuuwa lililofanywa na wanamgambo wa al-Shabab wenye mafungamano na al-Qaida. Radio ya taifa ya
Somalia na pia duru za kidiplomasia zimeeleza kuwa
msafara wa rais huyo umewasili salama katika bandari ya
Merka, baada ya shambulio hilo la kuvizia.
Al-Shabab ambayo ilikuwa ya kwanza kutangaza kutokea
kwa shambulio hilo, imesema imeweza kuharibu magari
kadhaa yaliyokuwa katika msafara huo.
Msemaji wa kundi hilo Abdulaziz Abu Musab ameliambia
shirika la habari la AFP kuwa shambulio hilo la kuvizia
limetokea karibu na kijiji cha Buffow, karibu na bandari ya
Merka, katika eneo ambalo lilikuwa ngome ya al-Shabab,
umbali wa km 100 kusini mwa mji mkuu Mogadishu.
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 MAONI :
Post a Comment