Pamoja na kwamba staa wa hiphop longtime kitambo P Diddy anakwambia hajakaribia hata kufikiria kuoa wakati huu ambao mwezi ujao anafikisha miaka 44 ya kuzaliwa, inaonekana amezama mapenzini kwa mtoto Cassie ambae ni mwimbaji.
Mwanzoni walikua sio wawazi sana kwenye mapenzi yao na hata wanapohojiwa walikua wakikwepa ila siku hizi mambo yamebadilika, hakuna siri tena na wamekua wawazi pia kupitia mitandao yao ya kijamii kama Instagram.
Basi hizi picha zinawaonyesha wakiwa nyumbani na mrembo Cassie akifanya foot massage na baadae wakiwa wamelala.
Kwa taarifa yako tu Diddy ni baba wa watoto sita na amewapata na Wanawake tofautitofauti.
Hizi hapa chini ni baadhi ya picha za Diddy akiwa na baadhi ya watoto wake.
0 MAONI :
Post a Comment