Tangaza na Abd Da Hustler

Wapinzani wa Kagame kuandamana Afrika.K


Karegeya alikuwa mshirika wa karibu sana wa Rais Paul Kagame kabla ya kutofautiana
Chama cha upinzani cha Rwanda National Congress leo kinatarajiwa kuandaa maandamano ya raia wa Rwanda wanaoishi Afrika Kusini hadi makao ya ubalozi wa taifa hilo mjini Pretoria kulalamikia mauaji ya aliyekuwa mkuu wa idara ya ujasusi Kanali Patrick Karegeya .
Karegeya alipatakina akiwa amefariki dunia katika hoteli moja mjini Johanesburg mwezi Disemba mwaka uliopita.
Wanaharakati wa upinzani kutoka Rwanda wanaoishi uhamishoni wamedai kuwa serikali ya Rais Paul Kagema huenda ndio iliyohusika katika mauaji ya bwana Karegeya.
Ubalozi wa Rwanda nchini Afrika Kusini umesema kuwa hautatishika na maandamano hayo.
Karegeya alikuwa mkuu wa zamani wa ujasusi nchini Rwanda, na alipatikana amenyongwa katika hoteli moja mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
Mjane wa Karegeya amesema kuwa atazikwa nchini humo.
Taulo iliyokuwa na damu ilipatikana katika chumba ambapo maiti ya Karegeya ilipatikana na polisi wanaendelea kufanya uchunguzi. Hata hivyo hakuna mshukiwa yeyote aliyekamatwa.
Muaji ya Karegeya, yamesababisha madai dhidi ya serikali ya Rais Kagame kusema kuwa huenda ilihusika na mauaji hayo.
Karegeya alikuwa mshirika wa karibu sana wa Kagame kabla ya kutofautiana naye.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment