Tangaza na Abd Da Hustler

Majambazi wavamia kituo cha polisi na kuua askari

Watu wanaosadikika kuwa ni majambazi waliojifanya raia wema walivamia kituo kidogo cha polisi cha Kimanzichana Pwani wakiwa na silaha za jadi na kumuua askari aliyetajwa kwa jina la Joseph Ngonyani alIyekuwa zamu na kuwajeruhi askari mgambo wawili.
Watu hao waliingia kama raia wema wanaohitaji msaada wa polisi lakini ghafla walimvamia askari huyo na kumkata mapanga kasha kumpora bunduki aina ya SMG ikiwa na risasi 30.
Watu hao walipora pia risasi za akiba 41.
Baada ya kujeruhiwa vibaya na watu hao marehemu Ngonyani alikutwa akiwa katika hali mbaya na kukimbizwa hospitali ya Wilaya ya Mkuranga ambapo alifariki wakati akipata matibabu.
Wengine waliojeruhiwa katika tukio hilo ni mgambo Mariam aliyejeruhiwa shingoni na kichwani, na mwingine aliyetajwa kwa jina la Venance aliyejurihiwa mgogoni kwa risasi.
Msikilize mwandishi wa Times Fm, Masau Bwire akiripoti kuusu tukio hilo na utamsikia pia Kamanda wa polisi wa Pwani.
Share on Google Plus

About Unknown

Naitwa Abdalla Ngowi, Napenda Michezo na kukupa habari mbalimbali kutoka katika kila kona ya ulimwengu huu!, karibu ABD da Hustler
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 MAONI :

Post a Comment